The State University Of Zanzibar

NORAD lazidi kuinyanyua  SUZA

Makamu Mkuu wa Wa Chuo Kikuu cha Taifa  cha Zanzibar (SUZA), Prof. Moh’d Makame Haji, ameelezea kuridhishwa na Shirika la Maendeleo la NORAD la Norway   linavyoendelea kuiunga mkono SUZA katika utekelezaji wa mairadi mbali mbali ya kitaaluma.

Katika mazungumzo yaliyofanyika  katika ofisi  za makao makuu ya  SUZA  Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja akiwa na Mratibu wa Miradi ya  NORAD Afrika, Grete Benjaminsen,   Prof. Haji alisema ushirikiano wao Shirika hilo  umeleta mabadiliko kwa kuwapatia fursa wafanyakazi na wanafunzi kujiunga na programu mbalimbali.

‘’Tunapata kuwezeshwa, wapo wanafanyakazi wengi wanafanya program kadhaa za  Uzamivu na Uzamili,  tuna furaha sana juu ya maendeleo haya’’, alisema Prof. Haji. Naye, Bibi Grete alieleza  kuwa Shirika lake linadhamini masuala ya kitaaluma katika nchi za Afrika na taasisi za utafiti na pia wanatafuta wadau watakaowaunganisha na SUZA ili kuijengea uwezo zaidi.