The State University Of Zanzibar

MJADALA SERA YA MICHEZO YA SUZA

MAKAMU Mkuu  wa Chuo Kikuu cha Taifa cha  Zanzibar (SUZA), Prof. Moh’d Makame Haji amewakumbusha  wadau wa Chuo hiki  kuzingatia kuweka  kipengele cha kulinda maadili na kutunza nidhamu  kwenye Sera ya Michezo ya SUZA.

Alisema washiriki wa michezo watambue  kuwa  wao ni wanafunzi wa SUZA  wakati wakiendelea na michezo walinde heshima zao, Chuo na nchi kwa jumla.

Alikumbusha kuwa suala la maadili ni vyema likaonekana kwa uwazi katika  sera hasa  ikizingatiwa kuwa  linahusisha muingiliano mkubwa  baina ya wanafunzi  na hata walimu ama wa ndani au  wa vyuo vyengine vya nje.

Akizungumza katika mjadala wa Sera ya Michezo uliofanyika makao makuu ya SUZA Tunguu mkoa wa Kusini Unguja  tarehe (21/03/2025), Prof Haji  alisema wakishiriki michezo yao wafahamu kuwa ni wanafunzi wa SUZA na watapaswa kusimamia misingi ya kinidhamu  na kuendelea  michezo katika kulinda maadili .

Alifahamisha kuwa michezo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  na Serikali ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania  ya   kuimarisha hamu ya vijana kushiriki, kuchangia maendeleo ya nchi na hasa kupata ajira hivyo kuna haja ya kuweka mfumo bora wa uendeshaji wa shughuli hizo.

 ‘’ Sera inafaa kuwa na kipimo kizuri cha kuwazingatia wanafunzi wanaoshiriki michezo endapo  ratiba  za masomo     zitaingiliana na muda wa masomo’’, alisisitiza.

 Alifafanua kuwa michezo ni jambo huru  ambalo halimbani mshiriki katika   masuala ya  kiimani wala kitamaduni ila kwenda kinyume na maadili ni jambo ambalo haliwezi kuvumilika.

‘’Tunataka watendaji na wanafunzi ambao wanahitaji kupata muda kuimarisha afya baina yao na taasisi nyengine kupitia michezo, kujenga uhusiano  na ustawi  bora ndani na  nje ya Chuo’’,  alisema   Prof. Haji.

 ‘’  Hii ni sekta muhimu katika sekta ya m kitaifa zinazoangaliwa kuongeza ajira ( fursa), kuburudisha kufurahi kukusanyika na kutoka nafasi ya kushiriki katika matukio mbali mbali

Aliongeza kuwa michezo ni sekta rasmi inayochangia  maendeleo ya nchi,  kuitambulisha kwa   kujenga ushirikiano mwema na kuiwezesha kujitangaza katika mambo mabli mbali.

Naye, Mratibu wa Michezo wa  SUZA wa ofisi ya Ustawi, Ndg. Hassan Khairalla, alisema SUZa ilikosa muongozo kwa muda mrefu na hivyo kuamua kutengeneza sera ili  Chuo kiendeshe mambo yake kwa utarabu wa kisheria.

Naye, Mwakilishi wa Kampuni ya Halotel, Daud Daud, ambaye ni mdau wa kwanza kujitokeza kushirikiana na SUZA katika sekta ya michezo alithibitisha kuiendeleza sekta na   hiyo kwa ushirikiano mkubwa.

Mapema Rais wa Serikali ya Wanafunzi ya SUZA, Bi Mwanamkuu  Jega Bakari ameushukuruuongozi wa wa SUZA kwa kuwa karibu na Serikali ya wanafunzi jambo linachangia kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

 Mkutano   wa kujadili Sera ya Michezo ya SUZA huu wa  wa wadau uliowashirikisha wanafunzi kutoka kampasi zote za chuo kikuu, wakuu wa taasisi za SUZA na wageni wengine walioalikwa kuchangia sera hiyo.