Chuo Kikuu cha Osaka cha Japan kimeifungulia milango ya kitaaluma Taasisi ya Chuo Kikuu
cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kwa kuwasaidia kujiunga na taasisi nyengine za zinazoatoa
programu za masomo ya Sayansi.
Akizungumza katika kikao maalum cha kujadili utekelezaji mkataba wa ushirikiano baina ya
vyuo vikuu hivyo, Msaidizi Mkuu wa Chuo cha Osaka anayefahamika kwa jina la Mwalimu Bi
Jamila alisema Chuo hicho kina vitivo kumi na moja ambavyo vinaongoza katika Sayansi na
taaluma nyengine ambazo kuna fursa za ufadhili zinatolewa.
“Sisi tuko tayari kuwasaidia kujiunga na vyuo vyengine kwa kuandaa mikataba mingine ya
ushirikiano”, alisema Mwalimu Bi Jamila.
Mapema Makamu Mkuu wa SUZA, Prof. Moh’d Makame Haji alisema kufuatia fursa za
kuwangunisha na vyuo vyengine nchini humo waliona kuwa Lugha ya Kiswahili ndio njia pekee
iliyowafikisha hapo walipo.
”Tuliona Kiswahili kitatuwezesha kushirikiana, tusingeweza kushirikiana nanyi kama hakuna
jambo leye tija kitaaluma ambapo Osaka walikuwa natafuta Chuo kinafundisha lugha ya
Kiswahili ikiwa ni lugha ya asili ya nchi hiyo”, alisema Prof. Haji.
Katika mkataba wa ushirikiano mnamo mwezi Julai walipoenda Japani kushiriki maonesho
walikubaliana ni kubadilishana wataalamu na wanafunzi wanaofundisha Kikorea na
wanaosoma Kiswahili na kushirikiana kwenye tafiti ambapo utekelezaji wa masomo unatarajiwa
kuanza mara tu baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Katika hatua nyengine, Mwalimu Bi Jamila alisema kuwa wanafunzi wa Uzamili na uzamivu
wana uwezo mkubwa wa kuwafundisha wanafunzi wazawa Kijapani na wako tayari kuja nchini
hata kama kibinafsi.
Katika mazungumzo hayo, Kumiko Miazaki, kutoka Idara ya Kiswahili ya Osaka alielezea
namna atakavyofanya tafiti za lahaja za Kiunguja katika Mkoa wa kaskazini Pemba na Kusini
Unguja.
Aliongeza kuwa video ya SUZA iliyooneshwa kwenye maonesho ya Japan ilisifiwa sana na
kuwavutia watu wengi ilionesha mbinu zinazotumika katika kufundisha lugha ya Kiswahili.
Alifahamisha kuwa wanataaluma wa Japan wana hamu kubwa ya kuja Zanzibar kufundisha
lugha hiyo na pia kujifunza Kiswahili.
Naye Mwalimu Ali Kassim Yussuf, Mkuu wa Idara ya Kiswahili alisema kuna mwamko mkubwa
wa Wajapani kujifunza Kiswahili ambapo inawezekana kutekekelezwa malengo yatu kwa
gharama nafuu.
Hivyo, alipendekeza njia rahisi ya kuwafikia wanataaluma kwa teknolojia ya kisasa inayoweza
kutumika kwa kwa pande zote mbili ambayo iliungwa mkono na ujumbe wa Osaka.
Kikao hicho kiliwashirikisha wakuu mbali mbali wa SUZA wakiwemo Bi. Shani Suleiman Khalfan
Mkuu wa Skuli ya Kiswahili kwa Wageni, Bi. Fatma Soud Nassor, Kituo cha Kimataifa cha
Taaluma za Uenezi, Bw. Abubakar Makame Fakih, Mkuu wa Skuli ya Kiswahili kwa Wageni,
Bw. Ally Kassim Yusufu , Mkuu wa Idara ya Lugha ya Kigeni, Bi. Kijakazi Omar Makame, Mkuu
wa Idara ya Kiswahili, Bw. Mtaib Omar Fakih, Mkuu wa Idara ya Sheria kilifanyika tarehe
26/08/2025 makao makuu ya SUZA, Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.