The State University Of Zanzibar

Bonga  yaitaka SUZA iwasaidie kufundisha Kiswahili Ethiopia

Chuo Kikuu cha Bonga kilichopo nchini Adis Ababa, Ethiopia kimekiomba Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar  (SUZA) kushirikiana nao  kuikuza taaluma hususan kuieneza lugha ya Kiswahili nchini humo.

Katika mazungumzo hao yaliyoushirikisha uongozi wa Chuo yaliyoongozwa na Mkurugenzi   wa Shahada  za Awali,  Dk. Khamis Haji Salum , Rais wa Chuo cha Bonga Dk. Petros  WOldegiorgis alisema  lugha ya Kiswahili imekuwa na wazungumzaji wengi ambapo  Chuo chake angependa kuwa sehemu ya kuimarisha lugha hiyo.

‘’Chuo ninachokiongoza kinafundisha lugha ya Kirusi  sasa nataka kifundishe na  lugha ya Kiswahili ambacho ndio utambulisho wa lugha za Afrika’’,  alisema Rais WOldegiorgis.

Aidha, aliongeza kuwa ana furaha kubwa sana kuona kuwa SUZA ni kituo kinachofundisha lugha ya Kiswahili jambo ambalo litasaidia kukuza ushirikiano  wa kitaaluma sambamba na  kubadilishana wataalamu wafanyakazi na wanafunzi, kufanya tafiti na kuimarisha utamaduni wa kiafrika.

 Rais WOldegiorgis alisema ana dira ya kuwepo Umoja wa Vyuo Vikuu  vya Afrika ambao utasaidia kuenzi falsafa za viongozi mashuhuri wa Kiafrika akiwemo Hayati Mwalimu Myerere na Kwame Nkuruma.

Alifahamisha kuwa Afrika ina kila historia, lugha, rasilimali utamaduni  mambo ambayo yanapaswa kusimamiwa na vizazi vilivyopo kwa  ambao wataunganishwa kupitia Umoja  wao kuwa kuzingatia falsafa za viongozi waliopita na

Nae Mkurugenzi  Haji alimueleza Dk.  Alimueleza Dk. WOldegiorgis  kuwa  SUZA haina haina pingamizi na ushirikiano wa kitaaluma kwani ndio dira inayochangia kuleta mabadiliko makubwa ya kitaaluma kwa kufanya tafiti za pamojan kubadilishana wataalamu.